Muundaji maudhui Warren ametangaza kuachana na mpenzi wake Whitney miezi chache baada ya wao kupata mtoto wao wa kwanza.
Kupitia video iliyochapishwa YouTube, Warren anasema kuwa yuko tayari kuondoka nyumbani na kumuachia Whitney nyumba yao kwa kuwa yeye anataka uhuru wake.
“Lakini siendi na chochote, namuachia kila kitu. Hii nyumba yote ni yake niataka tu uhuru wangu,”
Warren anasema kuwa aliona tabia za mpenzi wake zikiwa tofauti, kitu ambacho kilimfanya kuchukua simu yake na kuangalia aliyekuwa akizungumza naye.
Alipata kuwa Whitney alikuwa akimwambia rafiki yake shida zake, jambo ambalo halikumfurahisha kwa sababu haamini marafiki
“Binafsi mimi nina uzoefu mbaya sana na marafiki kwa sababu marafiki sio watu wa kuamini,”
Aliendelea na kusema kwamba alikuwa tayari kukaa kwa uhusiano lakini heshima haipo tena.
“Mimi nilikuwa tayari kukaa lakini msichana wenyu hanitaki. Alianza kunionyesha madharau, disrespect inaongezeka hapa na pale. Heshima haipo tena,” alisema
Warren alisema heri atafute chokoraa ampende kuliko kukaa na tajiri ambaye hampendi.
“Mimi nimetoka huko Kisii hata kama mimi ni chokoraa wacha nitafute chokoraa mwenzangu basi anipende kuliko kukaa na tajiri mwenye hanipendi,”
Pia alisema kuwa atamfanyia mwanawe chochote kwa sababu anampenda sana na kuwa hataki kufanya chochote ambacho kitamuathiri hapo mbeleni.
“Mimi yule mtoto nampenda na roho yangu yote. Nitafanya kitu chochote kwa hii dunia huyo mtoto aishi maisha fiti,”
Mashabiki walipoomuliza mahali Whitney yupo alisema kuwa yuko kwa nyumba ila hawaongeleshani.
“Ako hapa kwa nyumba nobody is talking to anybody,”
Warren alisema kuwa amevunjika moyo na anahitaji muda kufikiria kila kitu ambacho kimekuwa kikitokea.
“Mimi nimevunjika moyo vibaya sana na kwa hiyo sababu nataka kwanza nichukue muda nifikirie kuhusu kila kitu ambacho kimekuwa kikifanyika,”
Whitney alitangaza kuwa mjamzito akiwa mwaka wake wa kwanza katika chuo kikuu na umri wa miaka 19 kisa ambacho hakikupendeza watu wengi.
Warren na Whitney walijaliwa mtoto wa kiume miezi chache zimepita.