Siku ya Jumapili, Oktoba 20, wapenzi maarufu wa Kenya mwimbaji Kelvin Bahati na mwanavlogu Diana Marua waliadhimisha miaka minane ya uhusiano wao.
Wawili hao ambao wana watoto watatu pamoja walitumia siku hiyo kusherehekeana na pia kusherehekea safari yao ya mapenzi.
Katika ujumbe wake, Diana Marua alikumbuka jinsi mumewe alimpa zawadi kadhaa kubwa na kumlipia mahari mwaka mmoja uliopita.
"Leo, ukweli kwamba ni mwaka mwingine na wewe, ni Zawadi kubwa zaidi ambayo ningeweza kuuliza. Umeyafanya maisha yangu kuwa Mazuri sana, unanimwagilia maji kila siku, ninachanua kama ua bustanini. Umenipenda milele, na umefanya maisha kuwa ya thamani. Kila siku karibu na wewe ni Baraka ambayo siichukulii kirahisi,” Diana aliandika kwenye Instagram.
Mwanablogu huyo wa YouTube aliendelea kumhakikishia mumewe kuhusu jinsi anavyompenda sana na kumhakikishia kuwa anamtosha.
“Ndoto zetu ni Kubwa kuliko za jana na siwezi kusubiri kuuonyesha ulimwengu kile kinachotungoja mbeleni. Nina Wasiwasi na Nina Furahia Kinachokuja kesho. Tufanye hivi Babe, Tuishi maisha na kuyaishi kwa Utimilifu wake. ASANTE KWA YOTE,” alisema.
Diana pia alimtakia mumewe kumbukumbu njema ya mahusiano yao na akamwomba Mungu awaweke hai kwa ajili ya kila mmoja wao.
Bahati kwa upande wake alikuwa na ujumbe mfupi kwa mkewe Diana Marua ambapo alimtakia kumbukumbu njemaya mahusiano yao tu.
Pia alidokeza kuhusu kutaka kumpa mama huyo watoto wake watatu zawadi nane tofauti ili kuashiria hatua hiyo muhimu.
“Je, uko tayari kwa zawadi nane za kusherehekea hii ama niwache tu. Kheri ya kumbukumbu ya mahusiano mpenzi wangu,” Bahati alimwambia mkewe.
Katika majibu yake, Diana alimwambia, "Nataka tu kuzeeka na wewe, unatosha."
Wapenzi hao wawili walianza kuchumbiana mwaka wa 2016 na tangu wakati huo wamejaliwa watoto watatu pamoja.
Katika majibu yake, Diana alimwambia, "Nataka tu kuzeeka na wewe, unatosha."
Wapenzi hao wawili walianza kuchumbiana mwaka wa 2016 na tangu wakati huo wamejaliwa watoto watatu pamoja.