Ndambuki Mboloi aliaga dunia kwa ajili ya virusi hivyo siku ya alhamsi kimetangaza chama KMPDU.
Muungano huo sasa unaitaka serikali kuzindua huduma za kuwafidiwa wahudumu wa afya wanaoga dunia wakiwa kazini
Kufikia wiki jana Kenya ilikuwa imepoteza wahudumu wa afya 14 kwa ugonjwa wa Covid 19 huku zaidi ya 600 wakiambukizwa
Kwa ajili ya hilo KMPDU imezindua kampeini mtandaoni ili kutaka kuboreshwa kwa maslahi ya utendakazi ya wanachama wake wote .kampeini hiyo ni kwa heshima ya Daktari
Doreen Adisa ambaye aliaga dunia kwa ajili ya Covid 19
".. Mimi ni Adisa .. tunahitaji vitanda ,vifaa na huduma ya bima . afya yangu , maisha yangu kama daktari hayapo tena mikononi mwangu’ wamesema katika kampeini hiyo
Madaktari hao wameitaka serikali kuwalinda na kuwapa huduma za ushauri .
"Adisa alifanya kila alichoweza lakini ugonjwa huo ulimuangamiza . huku watu wengi wakiambukizwa ,madaktari zaidi wataambukizwa’
Wahudumu hao 14 wa afya walioaga dunia ni kutoka idadi ya watu 423 walioaga dunia kote nchini kwa ajili ya virusi hivyo kuanzia mwezi machi .Takriban wahudumu 768 wa afya wamepatikana na na virusi hivyo kufikia agosti tarehe 10 .