Daktari wa maradhi ya kupumua afariki Covid 19

Madaktari
Madaktari
Wahudumu wa afya wanaomboleza kifo cha mwenzao  aliyekuwa daktari wa maradhi ya kuumua ambaye alikuwa na ugonjwa wa Covid 19

Ndambuki Mboloi   aliaga dunia kwa ajili ya virusi hivyo siku ya alhamsi kimetangaza chama KMPDU.

Muungano huo sasa unaitaka serikali kuzindua huduma za kuwafidiwa wahudumu wa afya wanaoga dunia wakiwa kazini

Kufikia wiki jana Kenya ilikuwa imepoteza  wahudumu wa afya 14 kwa ugonjwa wa Covid 19  huku zaidi ya 600 wakiambukizwa

Kwa ajili ya hilo KMPDU imezindua kampeini mtandaoni ili kutaka kuboreshwa kwa maslahi ya utendakazi ya wanachama wake wote  .kampeini hiyo ni kwa heshima ya Daktari

Doreen Adisa  ambaye aliaga dunia kwa ajili ya Covid 19

".. Mimi ni Adisa .. tunahitaji vitanda ,vifaa na huduma ya bima . afya yangu , maisha yangu kama daktari  hayapo tena mikononi mwangu’ wamesema katika kampeini hiyo

Madaktari hao wameitaka serikali kuwalinda  na kuwapa huduma za ushauri .

"Adisa  alifanya kila alichoweza lakini ugonjwa huo ulimuangamiza . huku watu wengi wakiambukizwa ,madaktari zaidi wataambukizwa’

Wahudumu hao 14 wa afya walioaga dunia ni kutoka idadi ya watu 423 walioaga dunia kote nchini kwa ajili ya virusi hivyo kuanzia mwezi machi  .Takriban  wahudumu 768 wa  afya wamepatikana na  na virusi hivyo  kufikia agosti tarehe 10 .