DCI Kinoti amshtumu Murgor, Sarah Wairimu kwa Kutumia kesi yake kulipiza Kisasi

Mkurugenzi wa upelelezi wa makosa ya jinai George Kinoti amemshtumu Sarah Wairimu kwa kutumia mashtaka ya kesi inayomwandama kulipiza kisasi dhidi yake  na  wakili wake (Wairimu) Philip Murgor.

Kinoti analalamika kwamba madai yanayoibuliwa na Wairimu ni njama za kutumia mamlaka vibaya huku wakili huyo akitumia fursa hiyo kulipiza kisasi ambaye imekuwa ikidumu baina ya mkuu wa mwendesha mashtaka na mkuu wa upelelezi wa makosa ya jinai.

''Mahakama inafaa kufahamishwa kisheria kwamba  Sarah Wairimu na wakili wake Phillip Murgor  wamekuwa kabla, na baada ya kukamatwa, katika  kila chombo cha habari ikiwemo Youtube wakisimulia na kupeana mtazamo mbadala wa matukio kuhusu kesi hii, na iwapo kuna yeyeyote anayekiuka amri ya kortini ni hao wawili," alisema.

Aliendelea kudai kwamba mshukiwa anatumia kuendeleza juhudi zake za kujitetea katika kesi inayomkabili kuhusu kifo cha mumewe.

Akijibu madai hayo ya Wairimu, Kinoti anasema kwamba hiyo ni mikakati yake (Wairimu)  inayopangwa ya kujaribu kujitetea dhidi ya mashtaka.

Kinoti aliendelea kusema kwamba madai hayo yanakusudiwa na ni mikakati ya mshtakiwa na wakili wake kujitetea mapema kabla ya kesi yake kusikilizwa tena..

 Pia anadai kwamba ni mpango wa mshtakiwa kuwadharau  waendesha mashtaka na wapelelezi katika kesi yake.
 Mkuu huyo wa upelelezi anasema kwamba korti haina mamlaka ya kusikiliza madai hayo kwa kuwa waendesha mashataka hawakuhusishwa au kufahamishwa.

Isitoshe anasema kwamba korti haijatoa amri ya siku 30 kama jinsi inavyotakikana kabla ya kuzua madai mapya, aliongeza kusema kuwa Sarah alikuwa akiibua masuala ya urithi wa mali nje ya korti.

Kinoti anadai kwamba Wairimu na Murgor wanataka kutawala uchunguzi na mashataka ya kesi kama DPP na DCI huku sawia wakijitetea kama washtakiwa.