Dear KOT,' Itumbi awajibu wakenya kuhusiana na kuachiliwa kwa Jowie.

Wakenya almaarufu kama KOT jana wailitoa hisia mbalimbali kuhusiana na ujumbe wa Itumbi huku wakimwambia kuwa siku ya wapendanao imening'inia kwa sababu Jowie ameachiliwa.

Jowie alikuwa kuzuizini kwa zaidi ya mwaka mmoja kwa mauaji ya Monica Kimani, Jambo ambalo liliacha wengi wakifikiria kuwa Itumbi hataweza kuwa na Maribe kwa maana Jowie ameachiliwa.

Akiongea katika mahojiano na runinga ya kiss 100 Itumbi aliwajibu mashabiki na kusema,

"Kwa muda sasa sijasoma jumbe za KOT, na nina hakika kuwa wanasema niko kwenye shida kwa sababu Jowie ameachiliwa

Nafurahiya #KOT huu hapa ukweli mimi na Jacque Maribe ni marafiki wa dhati, kwa kweli uwa tunatembea sana na Jacque

Familia yake pia ni marafiki zangu hata marafiki zake ni wangu kwa hivo tutabaki kuwa vile." Alijibu Dennis.

Jana mashabiki wengi walijaza mtandao wa twitter kwa hisia zao kuhusiana na uhusiano wake Dennis na Maribe baada ya mshukiwa mkuu wa mauaji ya mwanabiashara Monicah Kimani kuachiliwa.

Mmoja wa mashabiki aliandika hisia zake,

"HATA NAJUA HUJASKIA VIBAYA. JOWIE AMEACHILIWA ON THE EVE OF VALENTINE. NDUGU ZILE POEM UTAKARIRIA NANI MSEE?. CHEST PAINS."

Wengine waliongeza hisia zao,

"THE RELEASE OF JOWIE IRUNGU GIVES JACQUE MARIBE A CHANCE TO RECEIVE A FOURSOME ON VALENTINE’S DAY."

Mwingine aliandika na kuuliza ni nani atakaye sherehekea na Maribe siku ya wapendanao.

"SO WHO TAKES MARIBE FOR VALENTINE’S DAY…JOWIE OR ITUMBI?"

Lakini unapoona umesoma yote na umesikia yote kumbe si hayo tu mmoja alisema na ujasiri kuwa

"JOWIE ATAPEWA TU UKIONA KWANZA VALENTINES."