Hivi majuzi, Zari alisema kuwa Diamond amemuachia majukumu ya kuwalea watoto wao wote wawili huku ikisemekana kuwa Diamond hajawahi watembelea watoto wao kwa muda wa miezi tisa iliyopita.
Jambo hilo lilitokea baada ya Diamond kupiga picha watoto wake wawili kupitia njia ya 'screenshot' alipokuwa anazungumza nao kupitia njia ya video.
Diamond amekanusha madai hayo alipokuwa akizungumza na vyombo vya habari kule nchini Tanzania,"Suala la malezi ya watoto halinishangazi mimi kwa sasa. Wazazi wanapopeana talaka mambo mengi huzuka na hasa ya watoto ila natumai kuwa kila kitu kitakuwa sawa hivi karibuni."
"Juzi nilikuwa katika sherehe za siku ya kuzaliwa na mjomba wa watoto wangu na zari alinipigia simu. Nilikuwa na mtoto wangu na Hamisa Mobetto na tulizungumza naye." Diamond alisema.