Akihojiwa katika chombo cha habari nchi jirani ya Tanzania, Diamond ametangaza kupiga kazi kubwa na Swaelee na Stefflondon.
”Nimefanya kazi nyingi za Kushikiana na wasanii, Nina collabo nyingi ndani hadi natamani nizitaje, Nina ngoma inakuja na @Swaelee, Kuna nyingine nimefanya na @Stefflondon”
Mwanaume huwa anaongeaga mara moja tu sasa ukitaka nikuweke uchi watu wajue unayonifanyia hata kwenye hilo tamasha hatokuja mtu sasa tuishie hapo nakutakia tamasha njema..."Alichapisha Kiba.
Inaonekana kuwa Ali Kiba anampa Diamond onyo awache kufanya mambo anayofanya la sivyo atatoboa siri ambazo watu wengi hawafahamu.
Letu ni kukaa kitako kuona vita vya fahali hawa wawili vitafikia wapi.
Katika mahojiano Diamond Platnumz alishangaa alichomaanisha Kiba,
"Niliona post ya Alikiba, sijui alilenga nini. Ni kaka yangu, ananizidi kwa umri, namheshimu sana."