Donald Trump amependekeza uchaguzi wa urais uahirishwe

Donald Trump amependekeza uchaguzi wa urais uahirishwe.

Donald Trump ametoa wito kuwa uchaguzi wa rais utakaofanyika Novemba uahirishwe akidai kuongezeka kwa upigaji kura kwa njia ya posta kunaweza kusababisha udanganyifu na matokeo yasiyo sahihi.

Kuna ushahidi mdogo wa madai ya Bwana Trump lakini kwa kipindi kirefu amekuwa akipinga upigaji kura kwa njia ya posta ambao anadai unaweza kusababisha udanganyifu.

Majimbo ya Marekani yanataka upigaji kura kwa njia ya posta kufanywa kuwa rahisi zaidi kwasababu ya wasiwasi wa matatizo ya kiafya kutokana na janga la corona.

Katika ujumbe wake kwa njia ya Tweeter, Bwana Trump amesema kupiga kura kwa njia ya posta kutafanya uchaguzi wa Novemba kuwa usio sahihi na wenye udanganyifu mkubwa katika historia ya nchi hiyo na aibu kubwa kwa Marekani.

Alisema hivyo bila kutoa ushahidi wowote kwamba kupiga kuta kwa njia ya posta kama inavyofahamika Marekani, kutahatarisha uchaguzi kuingiliwa na nchi za kigeni.

"Wanazungumza kuhusu uchaguzi kuingiliwa na nchi za kigeni lakini wanajua kwamba upigaji kura kwa njia ya posta ni njia rahisi ya nchi za kigeni kuuingilia," amesema.

Bwana Trump alisema njia hiyo tayari unadhihirisha kwamba hilo litakuwa matatizo tu katika maeneo ambayo imejaribiwa.

Mapema mwezi huu, majimbo sita ya Marekani yalikuwa yanapanga kufanya uchaguzi wa Novemba kwa njia ya posta: California, Utah, Hawaii, Colorado, Oregon naWashington.

Majimbo hayo yatatuma kura moja kwa moja kwa njia ya posta kwa wapiga kura wote waliosajiliwa, na baada ya hapo zitarejeshwa tena au kuwasilishwa siku ya kupiga kura - ingawa kupiga kura moja kwa moja bado kutakuwepo kwa wachache ambao hali italazimu kufanya hivyo.