Double agent? Diana Marua aeleza selfie yake na Victor Wanyama

Diana Marua  ni mwanamke ambaye ameyasikia yote na kuvumilia mashambulizi makali ya mtandaoni dhidi ya mume wake Bahati.

https://twitter.com/dianamarua_/status/1256220183884169219

Lakini hakujua kwamba atageuziwa mtutu wa bunduki na kuanza kujitetea akikimbia kuitetea hadhi yake baada ya kuibuka  madai kwamba wakati mmoja alikuwa katika uhusiano wa kimapenzi na mwanasoka Victor Wanyama. Madai hayo yalianzia twitter na picha zikaambatanishwa na madai hayo .

Katika  youtube, wakati wa maswali na majibu  ambapo alijumuika pia na mumewe Bahati  Diana amesema hakuwahi kuwa katika uhusiano na mchezaji huyo wa soka na kwamba walikutana kupitia kwa rafiki yao mmoja.

“ Nilikutana na Victor kupitia kwa rafiki na tukajivinjari kwa muda  na ndiposa zilipigwa zile picha’

Diana pia amewalaumu KOT kwa kuanzisha madai hayo  akisema waliamua kuzitumia picha za selfie pekee badala ya picha walizopigwa kwa makundi wakiwa watu wengi .

Bahati  alikuwa kimya  wakati mke wake akijitetea na kujaribu kuvunja madhara ya uvumi uliokuwa umesambazwa  na wanamitandao.

Bahati huenda ndiye akajilaumu kwa makombora ambayo mkewe anarushiwa kwani mwezi jana aliibuka na posti ya dharau kwamba hakuna mwanamume anayeweza kumtunza mke wake kwa sababu ni wa hadhi ya juu. Madai hayo ndio yaliyowachemsha wanamitandao waliozama na kuibuka na picha hizo za jadi za Diana  ili kumpa adabu Bahati kwamba kulikuwa na wanaume wengi mbele yake katika  maisha ya Diana kabla hajakutana naye.

MHARIRI: DAVIS OJIAMBO