DPP Haji aagiza kushtakiwa kwa Maneja wa kifedha wa KPA pamoja na mkewe,kakake kuhusiana na malipo ya Shilingi milioni 214.5

dpp
dpp
Mkurugenzi wa mashtaka ya  umma Noordin Haji ameagiza kushtakwa kwa  mneja wa kifedha wa KPA  Patrick Nyoike kuhusu ufiusadi unaohusisha malipo ya shilingi milioni 214.5 yaliyotolewa kwa njia isiofaa .

Katika Memo ya tarehe 10 mwezi Mei  Haji amesema  malipo hayo yalitolewa kwa  Nyali Capital Ltd (NCL). Amesema uchunguzi umefichua kwamba Nyoike aliitumia afisi yake kufanikisha  kuwekwa kwa NLC katika orodha ya kampuni za kulipwa pesa hizo kwa huduma na bidha ziliztolewa kwa KPA.

Haji pia amesema ushahidi umoenysha kwamba  hapakuwa na mkataba wowote kati ya   KPA  na Nyali Capital Limited  isopokuwa barua zilziotiwa saini na mamenaja wa KPA kwamba  KPA Ingetoa malipo   ya kuipa NLC fedha kutoka kwa kampuni  zilizokuwa  zikifadhiliwa na kampuni hiyo .

Kwa sababu ya hilo Haji amependekeza kushtakiwa kwa  Nyoike ,mkewe Jacinta Wambugu,  kakake  Alfred Hinga, Isaac Obunga (karani wa  KPA), Peter  Kinyanjui (mkurugenzi wa  NCL) na  Nyali Capital Limited. Mwezi uliopita  aliyekuwa Mkuu wa KPA Daniel Manduku  aliondolewa  mashtaka ya ufisadi  baada ya Haji kuktaa kuidhinisha mashtaka dhidi yake .

Alikuwa ameshtumiwa kw a kutoa tenda  ya ujenzi wa ghala la uhifadhi wa mizigo katika Nairobi Inland Container Depot (ICD) kwa njia isiofaa.Manduku alijizulu  mwezi uliopita .