Dry spell itanimaliza aki! Siwezi kutoka kwa boma langu ,Zari asema

NA NICKSON TOSI

Mataifa mengi barani yamechukuwa hatua za haraka za kuhakikisha kuwa hakuna wananchi wanaoranda randa mitaani ama kukutana na watu kihole baada ya virusi vya Corona kuathiri idadi kubwa ya watu .

Kwa watu wengine kama Zari Hassan huenda amri zilizotolewa na kiongozi wa taifa la Uganda Yoweri Museveni la kutaka watu wasitoke katika nyumba zao kama njia ya kupunguza visa vya kusambaa kwa virusi hivyo, ambavyo tayari vimeathiri baadhi ya watu Uganda litamuacha akiwa hana wateja .

Mama huyo wa watoto 5 alipokea barua kutoka kwa usimamizi wa nyumba ambayo anaimiliki ikimtaka kutotoka nje .

Zari amesema kutokana na tangazo hilo limemfanya hawezi kutoka nje kwenda kuwatembelea wapenzi wala wapenzi wake hawawezi kumjulia hali baada ya kupigwa marufuku ya watu kutembea.

Amehofia kuwa labda kibano hicho kitamfanya kukosa mtu wa kumpatia Lungula ya kutosha kwani wapenzi wake wanahofia kuwa labda watatiwa mbnaroni iwapo watatoka nje ya nyumba zao.