EACC yawaonya magavana kuhusu azimio la kuvinyima vyombo vya habari pesa za matangazo

pjimage (1)
pjimage (1)
Tume ya maadili na kupambana na ufisadi imewaonya magavana kuhusu uamuzi wa kuinyima kampuni ya Natio Media Group matangazo kwa ajili ya  habari zinazochapishwa na gazet la Daily Nation zinazowahusisha magavana wanaoshtumiwa kwa ufisadi .

Kupitia barua  kwa mwenyekiti wa baraza la magavana Wycliffe Oparanya ,afisa mkuu mtendaji wa Eacc Twalib Mbarak amesema kwamba uamuzi huo haufai na ni ukiukaji wa sharia na vipengee kadhaa vya katiba .

Katika barua yake Mbarak ameonya kwamba afisa yeyote wa kaunti anayetekeleza maagizo hayo kutoka kwa baraza la magavana atawajibikia binafsi hatua hiyo ikiwemo kushtakiwa  . Mbarak amemuonya Oparanya kwamba barua yake  ilikuwa ikitoa maagizo yanayokiuka sharia  na kwamba wote katika serikali za kaunti watakaotekeleza maagzo hayo wanajitioa katika hatari ya kuchukuliwa hatua za kisheria .

Baraza la vyombo vya habari , muungano wa wamiliki wa vyombo vya habari na chama cha  wahariri vyote vilikuwa vimekashifu hatua hiyo ya baraza la magavana dhidi ya kampni ya NMG.

Wamiliki wa vyombo vya habari jumatano walikuwa wametoa taarifa kulaani  uamuzi huo wa magavana na kusema kwamba hatua ilizochukua ina hatari ya kuvuruga uhusiano kati ya taasisi za umma na vyombo vya habari kado na kuweka mfano mbaya . Muungano huo ulisema COG  kama taasisi yoyote ya umma au mtu binafsi ina haki ya kulalamika kuhusu habari zinazochapishwa kuihusu  lakini kwa njia ifaayo . Taarifa iliyoleta utata  ilihusu magavana wanane ambao Eacc  inawachunguza kwa tuhuma za ufisadi .