Edwin Abonyo afunguka kuhusu kuoa baada ya Joyce Laboso kuaga

IMG_0245__1572358904_62856
IMG_0245__1572358904_62856
Aliyekuwa mume wa marehemu gavana Joyce Laboso amekana taarifa za kuoa.

"Sijafikiria kuhusu ndoa, ata kwa sababu mama ameenda nitafute mwingine haraka."

Katika mahojiano na kituo hiki, Abonyo amefunguka A-Z kuhusu maisha yake na Laboso.

Ni miezi tatu sasa tangu mama Loyce alipoaga dunia kwa makali ya gonjwa la saratani.

"Leo ni mwezi wa 3 kwa sababu alifariki tarehe 29..."

Kuhusu alivyohisi baada ya kumpoteza mpenzi wake, Abonyo alisema,

"Mapenzi na ule uwepo wa mama katika nyumba ni muhimu sana kwa familia na ni kitu ambacho yeyote amefiwa atakwambia..." alisema Abonyo.

Kuhusu kero la saratani, Abonyo amesema kuwa kuna wengi wanaumia kwa ugonjwa huu.

 "Kuna uchungu na ugumu sana. Niliwahi kupatana na wakenya wengi ambao wana ugonjwa huo..."

"Kuna wawili niliwahurumia niwalipia bill zao..."