Fahamu jinsi unavyoweza kutalii Kenya ,hata bila pesa nyingi

Watu wengi hutamani kutembea humu nchini maeneo kama,Mombasa, Maasai Mara na maeneo mengine mengi ilhali mfuko wao unawaangusha kwa kutokuwa na pesa.

Habari njema ndio hizi hapa jinsi ya kutembea na kutalii maeneo  uyapendayo katika bageti yako ama kama huna pesa ya kutosha.

1.Pika chakula kutoka nyumbani

Si wote ambao wanaweza nunua chakula cha hotelini ama nje, kama unapesa na unaweza nunua chakula hicho pesa hizo unaweza tumia kwa kitu kingine.

Pika chakula kutoka nyumbani ili kikuwezeshe katka utalii na kutembea kwako.

2.Tembea msimu ambao si wa utalii

Kila mmoja anafahamu kuwa msimu wa utalii viru na hata nauli ama kukomboa gari hupanda bei huku ikiwafanya wengi kutmia pesa nyingi katika utalii wao

Msimu ambao si wa utalii bidhaa na nauli huwa katika bei nafuu.

3.Ishi na kama wananchi wa kawaida

Endapo utafaulu kuenda kutalii maeneo tofauti nchini usiishi kama mtalii bali ishi kama wananchi wa eneo hilo ili husiuziwe vitu kwa bei ghali mno

Watu wengi huuza bidhaa kwa bei ghali endapo watakuona wewe ni mtalii wa eneo hilo.

4.Jua muda wa kutalii

Si wote ambao wanajua muda mwema wa kutalii au kupanga jambo fulani, endapo utachagua muda wako vibaya haya basi utalii wakona muda wako utakuwa umekwisha bure na kuharibu pesa zako.

5.Tembea na vikundi

Vikundi upunguza gharama ya kutalii kwa maana watu wengi hugawana gharama tofauti na kisha kufanikisha utalii wako.