" Naomba radhi mzee Omolo Awange kwa mimi kutoweza kufika ili kuhudhuria maazishi yako hata kwa lazima .Lakini nipo hapa nawe . Nafsi yangu ipo hapa nawe’ aliandika Miguna . Alimtaja baba mkwe wake kama mtu aliyependa kusoma kila aina ya vitabu pamoja na magazeti ."Mzee Molo Awange alisoma vitabu vyoye nilivyochapisha na makala nilioandika magazetini .Pia alifuatilia kwa karibu shughuli zangu zote katika vyombo vya habari’.
Pia alimshuru baba mkwe wake kwa kumruhusu awe mume wa binti yake kwa miaka 20. Aliahidi kuendelea kupigania haki zake na hatosalimu amri . Wakili wake John Khaminwa atawasilisha rufaa dhidi ya uamuzi wa kuisongesha mbele kesi yake hadi tarehe 23 machi . Khaminwa amesema mteja wake, Miguna anapitia mahangaiko huko ulaya .