Fears of a father! Diamond afichua kwanini anahofia mwanawe Tiffah kukua

Msanii Diamond Platnumz na aliyekuwa mkewe Zari Hassan wanaweza rudiana baada ya kutengana mwaka wa 2018, wawili hao hawajakuwa wakizungumza tangu waachane ilhali hivi majuzi wameanza kuzungumza kwa ajili ya wanawao.

Zari ni shabiki wa nyimbo za Diamond na amekuwa akijirekodi akisikiza nyimbo zake kisha kuweka kwenye mitandao ya kijamii.

Hivi majuzi aliwarekodi wanawe Tiffah na Nilan wakiucheza wimbo wa Diamond wa awali.

Msanii huyo alipost video hizo na kunakili ujumbe mfupi na kusema kuwa anahofia kuwa mwanawe Tiffah anakua kwa haraka.

#QTCHALLENGE FROM MY PRINCESS AND LOVELY DAUGHTER ❤🌺❤ @PRINCESS_TIFFAH 🌺❤🌺❤… HAKA KATOTO KAKIKUA KATANICHUNA SANA 😂." Aliandika Diamond.

Msanii huyo alipost video nyingine ya Tiffah na kuandika maelezo mafupi,

https://www.instagram.com/p/CAkTYuMjmpN/

"#QTCHALLENGE FROM MY GENIUS AND BELOVED DAUGHTER @PRINCESS_TIFFAH ALL THE WAY FROM THE SOUTH OF AFRICA….SHE KILLED EVERYBODY!"

Diamond naye hakusalia nyuma alipost video ya mwanawe Nilan akiucheza wimbo wake wa Quarantine.

"A #QTCHALLENGE FROM MY GENIUS PRINCE @PRINCENILLAN ❤🌺❤…. I BET THIS ONE IS GOING TO BE THE NEXT MARK ZUCKERBERG 🌍"