Fikra za kitoto! Viongozi wa dini ya Kislamu Mombasa wataka serikali ifungue misikiti

unnamed (24)
unnamed (24)
Viongozi wa dini ya kiislamu kata ya Mombasa sasa wanaitaka serikali kufungua Misikiti katika magatuzi ambayo yameandikisha visa vichache vya corona. Taarifa hizi zinajiri wakati ambapo wafuasi wa dini wanapokaribia kuadhimisha siku tukufu ya Idd - uL-Fitr baada ya mfungo wa Ramadhan hiyo kesho.

Serikali aidha imependekeza kuwa tarehe 25 Mei mwaka huu ambapo itakuwa Jumatatu kuwa siku ya kitaifa kwa maadhimisho ya siku japo ikawarai waumini wa dini hiyo kusherehekea nyumbani kama njia ya kuzuia watu kutangamana eneo moja.

Alhamisi, kamati kuu ya miungano ya waislamu nchini ilisema serikali ni sharti ifungue misikiti akisema wana uwezo wa kuzingatia masharti yaliyowekwa na serikali.

“If the government can trust drunkards enough to keep social distancing in eateries, then it should trust Muslims enough to open mosques for Idd prayers,” amesema Sheikh Juma Ngao.

Sheikh amesema ni kinaya  kuwadhamini watu walevi kwa kufungua maeneo ya burudani na kuendelea kufunga misikiti nchini.

na azimio la serikali la kutaka watu kuwa umbali wa kilomita moja

Ameongeza kuwa kaunti kama vile Kwale, Marsabit, Meru, Kisumu na Lamu zote zimesajili visa vichache vya maambukizi ya virusi hivyo.

Ametilia mkazo kuwa misikiti ambayo haitazingatia masharti yaliyowekwa na serikali ni sharti ifungwe .

Amesema katika kaunti za Nairobi na Mombasa ambapo visa vingi vimeripotiwa ni vyema misikiti kuendelea kufungwa japoa akasema kuwa maombi ni nguzo muhimu katika hatua ya kufanikisha vita dhidi ya corona.
“Prayers are an essential weapon against this pandemic. It is only through prayers that we can win against the Covid-19. And prayers done together are stronger than prayers done individually,” Sheikh Ngao amesema