Finaly:Serikali yatoa Shilingi Milioni 3 kujenga barabara ya Mwiki-Kasarani.

  Serikali  hatimaye imetoa shilingi milioni 300 za kuikarabati barabara ya Mwiki –Kasarani  baada ya mazungumzo ya muda mrefu  kati ya seneta wa Nairobi  Johson Sakaja na  maneja mkurugenzi wa maamlaka ya barabara za Mijini Silas Kinoti . Fedha zilizotolewa ni sehemu ya shilingi bilioni 1.7  ambazo serikali ilitenga kwa ukarabati wa kilomita 13 za barabara .

Wakati mkutano huo ,Sakaja amesema kundi la wajenzi wa barabara na vifaa vyao tayari vimetumwa katika eneo hilo na hatua zaidi zitafuata .  Hatua ya Sakaja kuingilia kati imejiri baada ya maandamano ya siku nne ya wahudumu wa matatu  wanaoitumia barabara hiyo ambao  wamekuwa wakilalamikia hali mbaya ya barabara hiyo . Tangu jumatatu  wahudumu hao ambao wamechoshwa na visa vya kila mara vya kuharibika kwa magari yao  waliizaba barabara hiyo  na nyingine zinazoelekea katika barabara kuu  ya Thika .

Wakaazi wa mtaa huo  wamelazimika kutembea kwa wiki nzima   hadi Roysambu  ambako wamechukua matatu  za kwuafikisha katikati mwa jiji . Hali mbovu ya barabara ya Kasarani kwenda Mwiki  imekuwa  kidinda sugu kwa wenyeji na maanadamano hayo sio mapya kwani yalianza hata wakati ya serikali za mabaraza ya miji kabla ya kuja kwa mfumo wa ugatuzi . Serikali ya kaunti ya Nairobi chini ya utawala wa  Evans Kidero  ilitumia shilingi milioni 500 kuifanyia ukarabati barabara hiyo  lakini baada ya miezi kadhaa wakaazi walirejelea maandamano kwa sababu ya kurejea kwa mashimo katikati ya barabara .