logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Morocco kuandaa mashindano ya klabu bingwa Afrika kwa wanawake

Morocco inaanda mashindano hayo kwa mara ya pili baada ya kuandaa mara ya kwanza mwaka wa 2022

image
na Brandon Asiema

Football17 October 2024 - 07:58

Muhtasari


  • CBE FC kutoka Ethiopia itawakilisha ukanda wa CECAFA baada ya kufuzu kipute hicho kwa kuishinda Kenya Police Bullets ya Kenya kwenye fainali.
  • Mashindano hayo yataandaliwa kuanzia Novemba 3 hadi Novemba 23 mwaka huu.

Shirikisho la soka barani Afrika CAF limetangaza Morocco kuwa mwandalizi wa fainali ya ligi ya mabingwa barani Afrika kwa wanawake Makala ya mwaka huu.

Nchi ya Morocco iliwahi kuandaa mashindano hayo mwaka wa 2022 ambapo timu ya ASFAR kutoka nchi hiyo ilinyakua taji hilo mwaka huo baada ya kuishinda Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini.

Timu sita zilifuzu kushiriki ligi hiyo kutoka kwa miungano minane ya soka kwa kuzingatia maeneo kigiografia katika michuano ya mchujo.

Mamelodi Sundowns walifuzu moja kwa moja kama mabingwa watetezi huku ASFAR wa Morocco wakifuzu kutokana na kuwa waandalizi wa kipute cha mwaka huu.

Katika ukanda wa Afrika mashariki na kati chini ya muungano wa CECAFA, timu ya wasichana ya CBE FC kutoka Ethiopia ilifuzu kushiriki klabu bingwa barani upande wa wanawake baada ya kuilaza Kenya Police Bullets  FC katika fainali ya michuano ya kufuzu makala ya mwaka huu.

Timu nyingine kutoka CECAFA zilizowai kushiriki mashindano hayo ni Vihiga Queens ya Kenya katika mwaka wa 2021, Simba Queens ya Tanzania mwaka wa 2022 na Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) ta Tanzania katika mwaka wa 2023.



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved