Aliyekuwa mchezaji wa zamani wa Gor Mahia na Harambee Stars
Austin Oduor maarufu kama Makamu, aliaga dunia Oktoba 16.
Beki huyo maarufu, alijiunga na Gor Mahia mwaka wa 1980
akitokea Luo Union.
Katika taaluma yake ya soka ya zaidi ya miaka 10, Makamu
ameshinda mataji mengi akitumikia timu hiyo, ikiwemo mataji ya bara Afrika na
taji ya ligi kuu nchini.
Aidha katika timu ya taifa, Austin Oduor atakumbukwa katika
michuano ya kufuzu AFCON ya mwaka 1990 akiwa nahodha wa Harambee Stars. Katika
mchuani huo, Oduor alipewa jukumu na kocha wake Mohammed Kheri kuhakikisha mshambuliaji
anayekisiwa kuwa bora zaidi barani Afrika George Wear wa Liberia hapati nafasi
ya kufunga bao.
Akiongoza wachezaji wenzake uwanjani kama nahodha, Harambee
Stars waliwafunga Liberia bao moja kwa nunge katika mchunuano wa kundi lao
lililojumuisha timu za taifa za Liberia, Egpyt na Malawi.