logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Ligi za kabumbu zarejea wikendi hii baada ya mapumziko ya kimataifa wikendi iliyopita

Ligi pendwa zaidi duniani EPL kuingia raundi ya 8 ya msimu wa 2024/2025

image
na Brandon Asiema

Football18 October 2024 - 08:06

Muhtasari


  • Manchester City inalenga kuendeleza msururu wa kutopoteza mechi ligi inapoingia raundi ya nane.
  • Mechi kubwa inayosubiriwa na wapenzi wa soka ni baina ya Liverpool na Chelsea siku ya Jumapili mwendo wa saa kumi na mbili na nusu.


Ligi za mbali mbali za soka duniani zinarejea wikendi hii baada ya mapumziko ya kimataifa wikendi iliyopita kupisha mechi za kufuzu makombe mbali mbali ya mabara duniani.


Ligi kuu Uingereza inarejea kwa mechi za raundi ya nane ya msimu huu, zitakazochezwa Jumamosi, Jumapili na Jumatatu.


Jumamosi 19, Tottenham itacheza dhidi ya West Ham mechi ya mapema mwendo wa saa 8 na nusu.


Jumla ya mechi tano zitachewa Jumamosi mwendo wa saa 11 ambapo Man United itakuwa nyumbani kumenyana na Brentford wakati Fulham itaialika Aston Villa. Everton itakuwa ugenini kucheza dhidi ya Ipswich Town wakati Newcastle na Southampton wakiwakaribisha Brighton na Leicester mtawalia wakati sawia.


Mikel Arteta na wachezaji wake watasafiri kuelekea uwanja wa Vitality ambapo watacheza dhidi ya mwenyeji wao Bournemouth saa moja na nusu jioni.


Jumapili, itakuwa zamu ya mabingwa watetezi Manchester City wakilenga kuendeleza msururu wa matokeo bora watakapocheza na Wolves saa kumi jioni kabla ya mechi inayosubiriwa zaidi wikendi hii kati ya Liverpool na Chelsea kuchezwa saa kumi na mbili Jumapili hiyo.


Aidha raundi ya nane ya msimu 2024/2025 itakamilika siku ya Jumatatu ambapo Nottingham Forest watakuwa nyumbani mwendo wa saa nne usiku kucheza dhidi ya Crystal Palace.


Ligi inaporejea, Liverpool inaongoza jedwali kwa alama kumi na nane, wakifuatiwa na Man City kwa alama kumi na saba. Nafasi ya tatu inashikiliwa na Arsenal kwa alama sawa na Man City, Chelsea ikitulia katika nafasi ya nne kumi na nne wakitoshana na Aston Villa wanaoshikilia nafasi ya tano kwa uchache wa magoli.

Manchester United inasuasua katika ukurasa wa pili wa jedwali la EPL wakiwakatika nafasi ya kumi na nne kwa alama nane baada ya mechi saba za msimu wa 2024/2025.


Nchini Uhispania, La Liga itaingia raundi ya kumi mechi zikiratibiwa kuchezwa kuanzia Ijumaa hadi Jumatatu.


Girona watacheza dhidi ya Real Sociedad Jumamosi saa kumi na nusu kisha saa nne usiku Celta Virgo kucheza dhidi ya Real Madrid. Barcelona watakuwa nyumbani kucheza dhidi ya Sevilla mwendo wa saa nne usiku.


Kwenye Bundesliga, Borussia Dortmund watacheza saa tatu na nusu Ijumaa usiku dhidi ya FC St. Pauli. Bayer Leverkusen watawaalika Eintracht Frankfurt saa kumi na nusu jioni wakati huo, RB Leipzig wakimenyana ugenini na Mainz nao Bayern Munich wakipambana na VfB Stuttgart.


Ligi ya Bundesliga inaingia raundi ya saba.




RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved