Wachezaji wawili wa raga walioshtakiwa kwa kumbaka mwanamke mmoja mwaka wa 2018 wameachiliwa kwa dhamana ya shilingi laki tatu pesa taslimu na hakimu wa Zainab Abdul.
Alex Olaba (23) na Frank Wanyama (22) waliokuwa wamehukumiwa kifungo cha miaka 15 jela walipata afueni baada ya mahakama kuagiza washtakiwe upya Juni tarehe 30.
Walipewa hukumu hiyo na hakimu mkuu Martha Mutuku Agosti mwaka jana. Mutuku alikuwa amewapata na hatia ya ubakaji.
Walishtumiwa kwa kumbaka mwanamke huyo ambaye ni mwanamuziki mwaka wa 2018 katika karamu moja mtaani Highrise.