Mbunge wa Starehe Charles Njagua al maarufu Jaguar amempiga vijembe mwenzake wa Embakasi mashariki Babu Owino ambaye azmeuiliwa katika gereza la Viwandani . Jaguar alipokuwa akitoa magodoro kwa wafungwa wa gereza hilo amesema Magodoro hayo pia yatamnufaisha mwenzake Babu ,ambaye yuko katika gereza hilo hadi jumatatu wiki ijayo.
" Leo nimetoa magodoro 2000 kwa wfaungwa wa gereza la Industrial Area .Naamini wafungwa wanastahili kuwa katika mazingira mazuri wakingoja uamuzi wa kesi zao.Mwenzangu Babu Owino pia ni miongoni mwa watakaonufaoika na magodoro haya ya ubora wa juu’ aliandika katika ukurasa wake wa facebook.
Babu ,siku ya jumatu alishtakiwa kwa jaribio la mauaji ya DJ mmoja Felix Odhambo kwa jina maarufu DJ Evolve katika eneo la burudani la B cLub . Picha ya CCTV katika eneo hilo la burudani inamwonyesha Babu akiitoa bastola yake na kasha kumfyatulia DJ Evolve . Babu amekanusha mashtaka dhidi yake na amewataka wakenya kungoja kusikia kisa chake kuhusu kilichotokea siku hiyo ." Nawahimiza wakenya kuwa watulivu na kungoja kusikiza upande wangu wa kisa hicho nikapotoka katika makao yangu ya sasa ya gereza la viwandani’ aliandika katika twitter .