FRENEMIES: Jaguar Atoa ‘Godoro’ kwa Babu Owino Gerezani .

JAGUAR AND BABU
JAGUAR AND BABU

Mbunge wa Starehe  Charles Njagua al maarufu Jaguar amempiga vijembe mwenzake wa  Embakasi mashariki Babu Owino  ambaye azmeuiliwa katika gereza la Viwandani . Jaguar alipokuwa akitoa magodoro kwa wafungwa wa gereza hilo amesema  Magodoro hayo pia yatamnufaisha mwenzake Babu ,ambaye yuko katika  gereza hilo hadi jumatatu wiki ijayo.

" Leo nimetoa  magodoro 2000 kwa wfaungwa wa  gereza la  Industrial Area .Naamini wafungwa  wanastahili kuwa katika mazingira mazuri wakingoja uamuzi wa kesi zao.Mwenzangu Babu Owino pia ni miongoni mwa watakaonufaoika na magodoro haya ya ubora wa juu’ aliandika katika ukurasa wake wa facebook.

Babu ,siku ya jumatu alishtakiwa kwa jaribio la mauaji ya DJ mmoja  Felix Odhambo kwa jina maarufu DJ Evolve katika eneo la burudani la B cLub . Picha ya CCTV katika eneo hilo la burudani inamwonyesha Babu akiitoa bastola yake na kasha kumfyatulia DJ Evolve . Babu amekanusha mashtaka dhidi yake  na amewataka wakenya kungoja kusikia kisa chake kuhusu kilichotokea siku hiyo ." Nawahimiza wakenya kuwa watulivu na kungoja kusikiza upande wangu wa kisa hicho  nikapotoka katika makao yangu ya sasa ya gereza la viwandani’ aliandika katika twitter .