Friends:Raila Afunguka kuhusu uhusiano wake spesheli na marehemu Joyce Laboso

Kiongozi wa chama cha ODM Raila Odinga  ijumaa alifunguka kuhusu  uhusiano wake spesheli na marehemu gavana wa Bmet Joyuce Laboso .Laboso,   kabla ya uchaguzi wa mwaka wa 2013 alikitema chama cha Raila ODM na kujiunga na mrengo wa naibu w arais William Ruto  wa chama cha URP  ambacho kilikuwa kimeteka siasa za Rift valley . Alikitetea kiti chake cha ubunge cha Sotika  ,hatua ambayo wengi wanasema ni kwa sababu ya hadhi  yake ,uadilifu  na rekodi nzuri ya maendeleo . Raila amesema ilikuwa vigumu sana kwa yeye na Laboso kuzungumza wakiwa nchini kenya kwa sababu walikuwa katika vyama pinzani ."Laboso  alishinda kiti cha Sotik lakini ilikuwa vigumu sana kwa sisi kuzungumza kwa sababu alikuwa katika chama hasimu’ amesema Odinga   wakati wa misa ya wafu ya Bi Laboso iliyofanyika katika uwanja wa Bomet .

Balozi huyo wa umoja wa mataifa  amesema walitangamana kwa muda na Laboso wakati wa kongamano la chama cha Democratic nchini Marekani mwaka wa 2016 .Raila  alimtaja Laboso kama binti yake  kwani alikuwa kielelezo kwake na mara nyingi Laboso  alitaka ushauri wa kisiasa kutoka kwake . Kiongozi huyo wa ODM alifichua kwamba  siku moja alimwambia Laboso kwamba angekuwa rais wa Kenya .

" Siku moja ,naona ukitoa hotuba kama rais wa kenya . nchini Kenya hatuwezi kuzungumza kwa kina lakini hapa tunaweza kuongea’ Raila alimwambia Laboso walipokuwa Marekani .Joyce  aliaga dunia siku ya jumatatu  katika Nairobi Hospital  baada ya kupambana na kwa muda mrefu na ugonjwa wa kanasa . Mwili wake umesafrishwa hadi  Fort Tenan ,Kisumu kwa maazishi ,Jumamosi .