Sifa zake hata hivvyo iso kuhusu uraia wa watoto wake bali alichofaulu kufanya ili kuwa na wanawe na maisha ambayo sasa anaishi kama malkia bila kufanya kazi . Esther hajawahi kugharamika hata kwa shilingi kuishi maisha yake ya kifahari kwa sababu baba za watoto wake hutuma pesa kila mwezi kwa matumizi ya wanao kuanzia karo ya shule , usafiri,kodi ya nyumba na chakula .kwa mwezi ,imedaiwa kwamba Esther hulipwa takriban shilingi nusu milioni na endapo kila baba ya mtoto wake angewajibika kwa kutuma pesa ,mwanamke huyo angekuwa akiingiza kitita cha shilingi milioni 1 kwa mwezi kama pesa za matumizi .
Sarakasi zake na wanaume zilianza alipkuwa akifanya kazi katika ubalozi mmoja wa taifa la kigeni na akiwa huko alijipata katika uhusiano wa kimapenzi na mfanyikazi mwenzake ,mzungu ambaye baadaye walipata mtoto naye na jamaa akarejea kwao . Licha ya kuachana mzungu huyop aliendelea kuwasiliana naye na hata alipojifungua jamaa alizidi kutuma pesa za matumizi ya mwanawe .Hapo ndipo Esther alipopata ujanja wa kuweza kupata pesa maisha yake yote bila kwenda kazini .
Kwa sababu ya kazi yake alikuwa akikutana na watu mbali mbali wengi raia wa kigeni katika balozi nyingine na muda sio mrefu ,alikuwa tena kapatana na mzungu wa taifa jingine ,kamuingiza boksi na kaboom! Alipata tena uja uzito na akazaa mwanawe wa pili .mzungu wa pili pia kaanza kutuma pesa na hapo ndipo Esther alipopata ujasiri wa kuzaa na wanaume wengine lakini wakenya waliokuwa pia na uwezo wa kifedha kugharamia mahitaji ya watoto wao kama walivyokuwa wakifanya wale wazungu.
Kamwe hakuolewa wala kuingia katika uhusiano wa wazi na yeyote kati yao lakini alizidi kuwatumia watoto kama chambo cha kuzidi kuvuna pesa kutoka kwa baba za watoto wake .
Magari anayobadilisha kila mara na ziara za holiday anazopiga Esther huwezi kuzimudu iwapo huna bunda la kutosha la mihela ,wengi wasiojua mchezo wake hata walimshuku kuwa muuzaji wa mihadarati lakini siri yake ilipogunduliwa ,Esther hakuwa na soni kwa sababu alionekana kufurahia maisha yake na mtindo aliochukua nao wanaume wale walifurahi kuendelea kugharamia maisha ya watoto wao ambao walikuwa chini ya paa moja . Dunia ina mambo!