Gavana wa Nandi Stephen Sang jumanne alishtakiwa kwa makosa matatu . Hakimu mkaazi Beryl Omollo aliyaaja mashtaka hayo kuwa uharibifu wa mali , uchochezi na kutumia vibaya maamlaka yake . Sang alikana mashtaka dhidi yake na mawakili wake kuitisha aachiliwe kwa dhamana .
Aliachiliwa huru kwa bondi ya shilingi milioni Moja na mdhamini wa kiasi kama hicho au bondi ya shilingi elfu 500 pesa taslimu .
Kwa uharibifu wa mali ,gavana huyo anashtumiwa kwa kuharibu sehemu ya shamba la Chai la Kibware juni tarehe nane . mashtaka ya uchochezi yametokana na matamshi yake kwa wafuasi wake kwamba wanafaa kujihami ili kuwapokonya mashamba watu walionyakuwa ardhi za umma likiwemo shamba la chai la Kibware .
Kwa kosa la kutumia vibaya maamla yake ,gavana huyo anashtumiwa kwa kutumia trekta za serikali ya kaunti ya Nandi wakati wa uharibifu wa mimea cha chai . Alilala seli katika kituo cha polisi cha Central mjini Kisumu baada ya kukamatwa na maafisa wa DCI huko Kapsabet.