Gavana wa Mombasa, Hassan Joho alazwa hospitalini

Gavana wa Mombasa Hassan Joho amelazwa katika hospitali ya Mombasa Hospital, mkurugenzi wake wa mawasiliano, daktari Richard Chacha amethibitisha.
Joho alijipeleka mwenyewe katika hospitali hiyo siku ya Jumatano na madaktari wakamuarifu kuwa anapaswa kuangaliwa kwa makini akiwa humo hospitalini.

Wadau wake wa karibu wanasema kuwa amekuwa akilalamika kuwa na homa isiyokuwa na mwisho.

Aliyekuwa rais wa Nigeria, Olesegun Obasanjo alimtembelea hospitalini Ijumaa mida ya mchana.

Tutakujulisha zaidi.