Gianni Infantino amechaguliwa tena kuwa Rais wa shirikisho la soka duniani Fifa katika mkutano wa wanachama wa shirikisho hilo la soka ulimwengui jijini Paris .
Infatino mwenye umri wa miaka 49 aliyechukua usukani katika shirikisho hilo mwaka wa 2016 baada ya kuondoka kwa Sepp Blatter hakupingwa kwa muhula mwingine wa miaka mine hadi mwaka wa 2023 .
Awali ,Infantino alisisitiza kwamba fifa limegeuzwa kuwa shirikisho linaloambatana na vigezo vya kuaminika na hadhi alipokuwa akiwahutubia wajumbe 211 wanachama wa shirikisho hilo .
" Leo hakuna anayezungumza kuhusu migogoro ,hakuna anayezungumza kuhusu kuijenga fifa kutoka chini wala sakata za ufisadi,tunazungumza tu kuhusu soka’ amesema mkuu huyo wa fifa ambaye awali alikuwa katibu mkuu wa shirikisho la UEFA .