Glavu zatolewa huku kambi ya Gideon Moi ikigawanyika

moi
moi
Kiongozi wa Kanu Gideon Moi huenda akajipata matatani endapo hatapiga hatua ya dharura kuwaunganisha viongozi katikamrengo wake Rift valley  baada ya kutokea mgawanyiko kabla ya uchaguzi kuu wa 2022 .

Hali imeonekana kuwa mbaya baada ya  mbunge wa cherengany  Joshua Kutuny kumshtumu Mi kwa kutojali maslahi ya watu wa Rift Valley .

Isitishe ,washirika wake wa karibu na wenye ushaiwishi katika chama chake  mbunge wa  Emurua Dikir Johana Ng’eno  na gavana wa West Pokot John Lonyangapuo -  wameonakana kuanza kuegemea upande wa naibu w arais William Ruto .

Ng’eno  ametangaza hadharani kwamba atamuunga mkono DP Ruto kugombea urais mwaka wa 2022 . Kulingana  naye toshi ya uongozi wa wakalenjin itaelekea Nandi mwaka wa 2022 kupitia Ruto kuisha ije kwa jamii ya Kipsigis

Gideon, ambaye ni seneta wa Baringo ni miongoni mwa viongozi wanalenga kumrithi rais Uhuru Kenyatta . Kutuny amesema alifiiri Gideon ni bora  zaidi ya Ruto lakini amegeuka kuwa  ‘mbwa mwitu katika ngozi ya kondoo ‘

Mbunge huyo  amekuwa mkosoaji mkubwa wa DP Ruto na hatua yake ya kubadilisha msimamo huenda ikawa na athari katika kambi ya Gideon Moi  . Ameliambia gazeti la the Star ;

“Gideon  sasa ni adui ya watu wa Rift Valley .Anawatambua maafisa wakuu watendaji katika mashirika ya serikali  kutoka Rift valley kisha kusababisha wafutwe kazi kwa madai kwamba ni washirika wa DP   Ruto’

Kutuny ndiye sura ya mrengo wa kielweke katika eneo la Rift valley  . tatizo lake la Gideon limetokana na mageuzi yaliofanywa katika shirika la KURA

Wote walikuwa wamekubaliana kwamba Luka Kimeli ambayealikuwa maneja mkurugenzi wa Kyura  na mkaazi wa cherangany  athibitishe kama mkurugenzi mkuuu wa maamlaka hiyo

Ha hivyo ,kulingana na Kutuny  ,Gideon alikiuka makubaliano hayo  yaliyokuwa yameidhinishwa na rais Kenyatta  na kushawishi uteuzi wa Philemon Kandie katika nafasi hiyo.Kandie anatoka Baringo