Guys! Wacheni nile bana, Hii corona ilinipeleka teke teke

7a6zSSeU.jfif
7a6zSSeU.jfif
Siku chache tu baada ya kuruhusiwa kurudi nyumbani baada ya kupata nafuu dhidi ya virusi hatari vya corona, mchungaji Margaret Wanjiru sasa ameamua kurejelea shughuli zake za kawaida.

Mbunge huyo wa zamani wa eneo bunge la Starehe alilazwa katika mashine ya ICU hospitali ya Aga Khan baada ya kupatikana na virusi hivyo.

Kupitia kwa ukurasa wake wa kijamii, Wanjiru amemshukuru Mungu kwa kuokoa maisha yake wakati alipokuwa amelazwa hospitalini na hata kutundika picha yake akiwa jikoni akiandaa mankuli.

"If the Lord was not on our side, the waters would have overwhelmed us but thanks be to God who always causes us to triumph," aliandika Wanjiru baada ya kuitundika picha hiyo.

Wanjiru aliruhusiwa kuondoka hospitalini mnamo Mei 30 mwaka huu ambapo alikuwa amelazwa kwa siku 9 kutokana na virusi hivyo.