Habari na Matukio Muhimu Unayofaa kujua kwa Sasa ,26th Septemba

RADIO JAMBO MIC
RADIO JAMBO MIC

WIZARA YA  elimu imefutilia mbali leseni za kuhudumu za shule mbili hapa nairpobi kwa ajili ya hofu kuhusu usalama wa shule hizo . waziri wa elimu  George Magoha ameagiza kufungwa kwa shule ya  Precious talent   mtaani dagoretti ambako wanafunzi wanane walifariki katika mkasa wa kuporomoka kwa jengo na  Pama academy mtaani kangemi . wanafunzi zaidi ya 400 waliokuwa precious talent watahamishwa hadi katika  shule za msingi za Ngong forest , jamhuri na  Riruta statellite . Mmiliki wa shule  ya precious talent  Moses wainana amekamatwa na atafikishwa kortini kesho .

kwingineko

Taarifa kutoka wizara imesema shule hiyo  imewasajili  wanafunzi wengi  kuliko idadi inayohitajika ,haina  vyoo vya kutosha hatua inayohatarisha afya ya wanafunzi  na imejenga  majengo yasio salama kwa wanafunzi . maneja wa shule hiyo pia ametajwa kama asiyehitimu kuisimamia .

Mahakama  moja hapa jijini imekataa ombi la  mkurugenzi wa mashtaka ya umma kubadilisha masharti ya bondi ya mfanyibiashara  Humphrey Kariuki  ili aweze kuzipata paspoti zake . DPP  alitaka kariuki arejeshewa dhamana ya shilingi milioni 11  aliolipa kama pesa taslimu  na badala yake atoe bondi ya thamani ya juu  lakini mahakama imesema kariuki atalipa bondi itakayohakikisha kwamba atarejea kortini kuhudhuria vikao vya kesi yake .

Maafisa wakuu wa usalama katika kaunti ya Kiambu wamehamishwa mara moja kufuatia ongezeko la visa vya uhalifu katika eneo hilo  .waziri wa usalama wa ndani Fred matiangi amesema watakabiliana na magenge ya uhalifu katika kaunti hiyo bila huruma .

 Mswada wa  Punguza Mizigo umekataliwa na bunge la kaunti ya Kisii  na kuwa kaunti ya tano kuukata mswada huo . waakilishi wadi waliutaja mswada huo kama wa kupoteza muda  na unaohujumu jitihada za kuzidisha uakilishi . kaunti za kirinyaga ,homabay ,nyamira  na muranga ndizo ziliukata mswada huo wa irdway Alliance ilhali  Uasin Gishu ndio kaunti pekee iliyoupitisha .

Siku moja tu baada ya afisi ya fedha ya kaunti ya busia kuteketea kwa njia ya kutatanisha, maafisa wa tume ya kupambana na ufisadi nchini EACC wamevamia afisi ya gavana na kuchukua stakabadhi kadhaa.Maafisa hao saba walioandamana na maafisa wa upelelezi kutoka kaunti ya busia wamepiga kambi katika afisi hizo na kuonekana wakipekua stakabadhi kabla ya kuondoka  nazo

Mahakama imemzuia gavana wa uasin Gishu Jackson Mandagapo dhidi ya kuongeza kodi ya ardhi . kaunti hiyo imepewa siku 14 kusuluhisha utata kuhusu  suala hilo  .Mandago hata hivyo  amekanusha madai kwamba kodi ilitaka kuongezwa

Sarah Warimu,  mjane wa bwenyenye mdachi marehemu Tob Cohen  amehoji wajibu wa mkuu wa DCI George Kinoti  katika kesi nzima ya mauaji ya mumewe .kupitia  waraka aliowasilisha leo kortini ,wairimu amezua mswali kuhusu wajibu wa kinoti kuhusiana na  mali alioachiwa dadake  Cohen Gabrielle Van Straten.  Kulingana na wairimu ,jukumu la Kinoti ni kuchunguza kesi ya uhalifu na sio  umiliki wa mali .

Mmoja kati ya wanawake kumi Mombasa anataka kutumia dawa za kupanga uzazi lakini wengi hawawezi kuzipata dawa hizo . mkurugenzi wa afya katika kaunti hiyo  Shem Phata  amesema ni asilimia 55 ya wanawake ndio hutumia njia au dawa za kupanga uzazi .

Gharama ya dawa nchini ipo juu sana na kuna haja ya kuthibiti  bei ya dawa ili kuhakikisha kwamba gharama ya jumla ya huduma za afya inapungua . Dr Kamamia Murichu  kutoka kwa muungano wa wasambazaji wa dawa  amesema dawa za humu nchini huuzwa hadi asilimia 200 zaidi ya bei katika mataifa mengine .

Polisi wamenasa  mikebe 68bya plastiki iliyokuwa na cocaine pamojana sachet kadhaa za bangi mtaani riruta . oparesheni hiyo pia ilipelekea kupatikana kwa biskuti zilizotegezwa kwa dawa hizo .washukiwa wawili wamekamatwa na watafikishwa kortini .

MJANE WA bilionea Marehemu Tob Cohen Sarah Wairimu atasalia rumande hadi jumanne wiki ijayo  baada ya kukosa kujibu mashataka ya mauai dhidi yake kufuatia ripoti kwamba wakili wake Philip Murgor ni  na wakili wa  mashataka wa serikali . jaji stela Mutuku amesema  sarah atajibu tu mashjtaka dhi yake wakati suala hilo litaposuluhishwa .

Polisi wamenasa  dola bandia za kimarekani na  vipande 147 vya dhahabu Feki katika eneo moja la burudani mtaani kilimani hapa jijini . mmiliki wa eneo hilo  amekamatwa .

Rais Uhuru Kenyatta amewarai  wanachama wa umoja wa mataifa kuipigia Kenya kura  katika azma yake ya kutaka kuwa mwanachama asiye wa kudumu katika baraza la usalama la umoja wa mataifa  kwenye uchaguzi ukaofanyoka juni mwaka ujao . rais amesema Kenya imedhihirisha mchango wake katika kuleta amani  duniani na kukabiliana na changamoto nyingine za kiusalama .

Serikali imesema itakabiliana vikali na wahalifu  ambao wanawahangaisha wakaazi wa kiambu .waziri wa usalama wa ndani Fred Matiangi  amesema atatekeleza mabadiliko katika  idara za usalama katika kaunti ya kiambu .

Kuna ongezeko la idadi ya vijana wanaotumia mihadarati na pombe huko eldoret .kamishna wa kaunti ya Uasin Gishu    Abdirizack Jaldesa amesema wamezidisha msako wa kuwakamata wanaouza dawa za kulevya kuwatumia watoto wa kuranda randa mitaani .