Mwalimu kuanguka na kuaga dunia kwa hali isiyojulikana

Polisi mjini Mwatate kaunti ya Taita Taveta wanaendelea na uchunguzi kubaini kilichosababisha kifo cha ghafla cha mwalimu mmoja wa shule ya upili ya kitaifa ya Bura Girl's huko Mwatate.
Inasemekana Walter Odhiambo alizirai na kuaga dunia punde tu alipofikishwa katika hospitali ya Mwatate na walimu wenzake.

Akithibitisha kisa hicho afisa mkuu wa polisi mjini Mwatate Monicah Kimani alisema ripoti ya upasuaji itaeleza rasmi sababu ya mauti ya mwalimu huyo.
Swali ni je mwalimu huyo alifanya nini na ni nini kilicho mfanya afariki?

Mwili wa mwenda zake unahifadhiwa Katika chumba Cha kuhifadhi maiti Cha hospitali ya st Joseph Shelter of hope Ikanga mjini Voi huku ukisubiri kufanyiwa upasuaji.