Mpenziwe Rayvany, Mama Fahima amefichua kwamba amebadilisha imani yake kutoka Uislamu hadi Ukristo. Fahima alisema hayo kwenye mahojiano na kituo kimoja cha televisheni nchini Tanzania.
"Nimebadilisha imani yangu sio kwa sababu ya kutaka kuolewa ila nimebadilisha kwa kuwa bwanangu na watoto wangu ni Wakristo. Nyanyangu alikuwa mkristo huku mamayangu alilelewa ndani ya familia ya Kikristo."
Alipoulizwa kuhusu tendo la kufunga pingu za maisha,"Ndoa ipo ila ningependa watu wawe na uvumilivu kwa sasa." Fahima alisema. Kwa sasa Fahima na Rayvanny wana mtoto mmoja.
Kwenye imani ya kiislamu,tendo la kubadilisha imani halikubaliwi. Hata hivyo, mashule kadhaa ya imani hii huwa na maoni tofauti tofauti kuhusiana na tendo hilo.