Offside au Red card? Jina la Mariga   halipo katika sajili ya wapiga kura ya IEBC .

 

Aliyekuwa mchezaji wa Harambee stars McDonald Mariga  amepata pigo katika jitihada zake za kutaka kuwa mbunge wa Kibra  baada ya kugundulika kwamba jina lake halimo katika sajili ya wapiga kura ya IEBC . Afisa wa IEBC Beatrice Muli  amemwambia Mariga kutafuta usaidizi kutoka kwa  bodi ya kusuluhisha mizozo ya IEBC .

" Tumefutilia mbali  uteuzi wa Mariga’ amesema afisa  huyo .Hata hivyo stakabadhi nyingine alizowasilisha kwa  IEBC zipo sawa . Mbunge wa Lang'ata Nixon Korir  na aliyekuwa seneta wa Kakamega Boni Khalwale  walijaribu kumshawishi kamishna wa IEBC kutumia muda wake wa kutosha kuliangalia jina la Mariga katika sajili .Mariga  ana siku saba kukata rufaa dhidi ya  uamuzi wa kumfungia nje ya uchaguzi huo . Chama cha Jubilee  awali jumanne kilikuwa kimemkabidhi Mariga cheti cha uteuzi .

"Kazi ianze sasa..imebaki kwenda kwa mafans. Mariga  alisema wakati alipokabidhiwa cheti cha Jubilee

Walioandamana naye ni  Didmas Barasa (Kimilili), Caleb Kositany (Soy),  na  Gladys Shollei (mwakilishi wa akina mama wa Uasin Gishu).