Wazazi katika shule ya msingi ya kakamega ambao wanao 15 waliaga dunia baada ya tukio la mkanyagano watangoja kwa muda kabla ya kufahamu kilichosababisha vifo vya watoto wao wiki mbili zilizopita . watoto hao tayari wamezikwa lakini polisi wanaendelea na uchunguzi ili kujua kilichotokea siku hiyo . Shule hiyo ilifunguliwa tarehe 10 februari baada ya kufungwa kwa wiki moja . sababu kadhaa zimetolewa ili kueleza kilichofanyika siku hiyo lakini hakuna iliyothibitishwa kuwa halisi iliyowafanya watoto hao kukimbia na kuanguka wakitoka katika madarasa yaliokuwa katika jengo la gorofa .
Sababu hizo ni pamoja na ripoti kwamba watoto hao walishtuliwa , kuwepo imani ya kuabudu mashetani na kwamba mwalimu mmoja alikuwa na kiboko akitaka kuwachapa watoto hao . Makachero hasa wanamtaka Seneta wa zamani wa kakamega Bony Khalwale kutoa maelezo kuhusu madai yake kwamba kuna madhehebu ya kuabudu mashetani shuleni humo .
Akizungumza na walimu ,wazazi na wanafunzi wa shule hiyo tarehe 4 Fberuari,Khalwale alizua maswali kuhusu imani za baadhi ya makanisa ambayo hufanya maombi shuleni humo siku za jumapili . Mkuu wa DCI katika eneo la magharibi Shem Nyamboki amesema pindi uchunguzi wao utakapokamilishwa ,watawasilisha faili ya mapendekezo yao kwa afisi ya DPP kwa hatua zaidi kuchukuliwa .