COVID 19: Polisi wawatawanya waumini makanisani Mombasa

Polisi siku ya jumapili walipata ugumu wa kuwazuia  Wakiristo nyumbani  mjini Mombasa  huku kaunti za pwani zikizidisha juhudi za kukabilianba na virusi vya Corona .

Maelfu ya  waumini waliwasili katika makanisa mbali mbali kwa misa za jumapili bila kujali kuhusu agizo la serikali kuwataka watu kuepuka maeneo yenye umati .  Baadhi ya makanisa tayari yalikuwa yamefanya misa ya kwanza mwendo wa  wa saa kumi na mbili unusu alfajiri .

Vikosi vya maafisa wa usalama  viliwasili katika kaisa la  Jesus Celebration Centre  huko  Bamburi  na kanisa la katoliki la  Holy Ghost Cathedral  katikati mwa jiji kuwatawanya watu .  Katika kanisa la JCC Buxton,  misa ya kwanza kati ya  6.30am  na  8.30am ilifanyika kama kawaida .Polisi waliikatiza misa ya pili kuanzia saa mbili unusu asubuhi hadi  saa tatu unusu .