Aluta Continua: Uhuru sasa kuwafurusha washirika wa Ruto Katika kamati za senate

Siku chache baada ya kuwaondoa  uongozini maseneta wanaomuunga mkono DP William Ruto katika senate , mpango wa kuwafurusha maseneta wa mrengo wa Rutro katika kamati za senate sasa umeanza kutekelezwa .

Mtikisiko mkubwa wa uongozi wa kamati hizo unatarajiwa kufanywa kufikia siku ya jumanne . Kiranja  wa upande wa walio wengi Irungu Kang’ata  amesema wanakamilisha mabadiliko hayo na wanatumai kwamba yatakuwa tayari kufikia siku ya jumanne .

Miongoni mwa wale wanaolengwa  ni maseneta saba  waliopinga hoja ya kumuondoa Kindiki Kithure kam naibu wa spika  wa senate .

Maseneta hao ni  Kipchumba Murkomen (Elgeyo Marakwet), John Kinyua (Nyandarua), Samson Cherargei (Nandi), Susan Kihika (Nakuru), Aaron Cheruiyot (Kericho), Benjamin Langat (Bomet)  na  Kindiki mwenyewe .

Siku ya ijumaa  maseneta wote wa Jubilee  isipokuwa saba  hao  walipiga kura ya kumfurusha  Kindiki kama  naibu wa spika wa senate  baada ya jumla ya maseneta 54 kuidhinisha hoja hiyo .

Kindiki  alifurushwa  kwa kutokuwa muaminifu kwa rais Uhuru Kenyatta ambaye ndiye kiongozi wa chama cha Jubilee .

Kang’ata hata hivyo amesema  hapatakuwa na hila dhidi ya jamii yoyote katika kupendekeza mageuzi  hayo katika senate  lakini akaongeza kwamba baadhi ya waliopinga hoja hiyo watakiona cha mtema kuni.Cheruiyot  yupo katika kamati ya PSC ,ambayo ni muhimu kwani huta maamuzi  bungeni .pia ni mwanachama wa  kamati za ICT, Kawi na Bajeti

Kinyua, Cherargei  na  Langat  ni wenyeviti wa kamati za senate  na huenda wakapoteza nafasi hizo .Kinyua  ni mwenyekiti wa kamati ya ugatuzi  na uhusiano kati ya serikali kuu na za kaunti   na pia ni mwanachama wa kamati ya afya.

Charargei  ni mwenyekiti wa  kamati ya haki  ,masuala ya kisheria na haki za binadamu  ambayo wanachama wake ni pamoja na   James Orengo  na  Okong’o Mogeni (Nyamira). Cherargei  pia ni mwanachama wa kamati za ugatuzi na leba .

Langat ni mwenyekiti wa kamati ya elimu  .seneta huyo wa Bomet pia ni mwanachama wa  kamati ya shughuli za bunge   na kamati ya kanuni na utaratibu . Pia yupo katika kamati ya  Utalii na viwanda .