Chelsea kuchuana na Arsenal katika fainali ya FA baada ya kuitinga Man U 3-1

CHELSEA
CHELSEA
Kilabu ya Chelsea itachuana na arsenal kwa fainali ya kombe la FA  baada ya kufauu kuishinda Manchester United mabao matatu kwa moja uwanjani Wembey katika mechi ambayo mlinda lango David De Gea  alipitia masaibu makubwa  baada  ya kushindwa kwa timu yake .

Kocha wa United Ole Gunnar Solskjaer  alimuacha mkekani mlinda lango wake wa mechi za FA  Sergio Romero  ili kumpa De Gea kazi hiyo  lakini masihara yake mawili yaliwafanya kushindwa  kwani aliizawadi Chelsea mabao mawili

De Gea  alifanya mchezo  kujaribu kuokoa mkwaju wa Olivier Giroud katika kipindi cha kwanza kisha tena akatapatapa na mkwaju wa yadi 20 wa Mason Mount  muda mfupi baada ya kipindi cha pili kuanza .

Mchezo mzuri wa Chelsea ulipigwa jeki wakati  nahodha  Harry Maguire alipojipata amewavua mkwaju wa   Marcos Alonso katika lango lake zikiwa zimesalia dakika 16 mchuano kutamatika .

Kikosi cha Frank Lampard Kilikuwa na uthibiti kamili kuanzia mwanzo wa mechi hiyo  na walifaulu kumaliza msururu wa man unitedwa kutoshindwa katika mechi 19 kwenye mashindano yote .

Bruno Fernandes aliifungua the reds bao moja  kupitia penalti lakini  halikufuta chochote kwa sababu wino ulikuwa umeshakauka .