Ukatili:‘Alinimuagia Acid katika sehemu zangu za siri nilipokatiza uhusiano wetu’

pjimage
pjimage
Teresa kipchumba amekuwa nje na ndani ya hospitali kwa mara zaidi ya anazoweza kukumbuka baada ya kupatwa na tatizo baya sana la kiafya wakati mwanamme  waliyetenganaye naye alipomwagia tindi kali au aci katika sehemu zake za siri .

Safari yake ya kupona na kupata haki imekuwa ndefu na yenye machungu kwa sababu  kando na  pesa nyingi anazotumia kuwa matibabu yake ,mshukiwa alikwepa  na kwenda Sudan Kusini alipomfanyia unyama huo .

Teresa anasema ulimwengu ulimpindfuka na kumuacha hoi miaka miwili iliyopita wakati mazungumzo yasio na hila kati yake na mwanamme huyo ili kukatiza uhusiano wao yalipotumbukia  kuwa janga kwake .Anasema wakati walipoanza uhusiano hakujua kwamba jamaa huyo kwa jina Japheth alikuwa na mke . Baadaye alipofahamu ukweli  kwamba Japheth alikuwa na mke ,Teresa alimtaka wakatize uhusiano wao lakini kumbe Japheth hakulichkulia kwa wepesi suala hilo  na baadaye akapanga jinsi ya kumuadhibu Teresa akimlaumu kwa kuhitimisha uhusiano wao.

Japheth siku chache baadaye alimvizia  Teresa akiwa nyumbani kwake na kummininia  acid kwenye sehemu zake siri baada ya kumzidi nguvu na kumtoa nguo . pindi baada ya ukatili huo wake alitoroka na baadaye ikaripotiwa kwamba alikimbilia nchi jirani ya Sudan Kusini alikokuwa akifanya kazi . Baada ya tukio hilo Teresa alianza  safari ndefu ya kuanza  matibabu kwani acid hiyo ilimdhuru ngozi katika uke wake na kumfanya kuhitaji upasuaji maalum .

Anasema  uchungu aliyopitia akipokea matibabu tangu sasa  humfanya wakati mwingine kutaka kujiua lakini jamaa zake na rafiki zake wa karibu ndio wamekuwa wakimpa himizo la kuendelea kutaka kuishi . Aliwekea vifaa maalum vya kwnda haja ndogo na dawa ambazo  yeye hupewa kila mara kutuliza maumivu  zinamfanya kupata matatizo mengine  kama vile kupoteza fahamu . Anasema katu hajawahi kusikiza mwanamume aliyechukulia kwa hasira habari za kuchwa na mpenzi wake na kuamua kuchukua hatua kama hiyo na tangia tukio hilo Teresa ameapa kwamba hatowahi tena kupenda .