Pastor alivyowakula ‘kondoo’ na kupelekea kanisa kufungwa

  Maajuzi  amezua mheko raia mmoja wa kigeni ambaye aliziweka mtandaoni picha  zake akiwa an wanawake kadhaa wa kenya anaodaiwa kulala nao .Lakini wanachosahau watu wengi ni kwamba kama mzungu huyo kunao watu kadhaa hapa nyumbani walio pia na tabia hiyo . Mmoja ni jamaa mmoja aliyekuwa ana kanisa lake  katka mtaa wa Ongata Rongai ambalo lilibomolewa na waumini waliodai kwamba alikuwa amelala na wake zao na wasichana wote wa kanisa hilo .

Mhubiri huyo ambaye kwa sasa alihamia mji mwingine na kufungua kanisa kutumia jina tofauti mwaka wa 2017 alidaiwa  kuwapachika mimba wanawake 12 wa kanisa lake na kati yao 7 walikuwa ni wanawake katika ndoa zao . Maandamano makubwa yalizuka wakati tabia yake ilipogunduliwa na watu wa kanisa hilo na kwa pamoja jumapili moja walilivamia kanisa hilo na kulibomoa huku mhubiri akiponea kwa kutoroka kupitia mlango wa nyuma .

Baadaye wanawake wengi ambao hawaku wameolewa walisimulia jinsi alivyowahadaa kwamba atawaoa  na pindi waliposema wana  mimba yake aliwapa pesa wazitoe mimba  na kuruka kwa msichana wa pili kanisani ambaye pia baada ya muda alijiata katika hali kama  hiyo .

Kuna wanawake ambao waliachwa na waume  zao baada ya ufichuzi huo kutolewa kuhusu walivyokuwa  wakilala na mhubiri .Wale waliojifungua watoto ,ambao walidaiwa kuwa wa mhubiri huyo waliachwa na waume zao na hadi leo hajawahi kuajibikia vitendo vyake .Jaribio la baadhi ya wanawake hao kutaka mahakama iwasaidie ili jamaa atoe pesa za kuwalea wanao zimegonga mwamba .

Katika mji alikohamia ,jamaa alijenga kanisa jipya huku wenyeji wasijue mbona alikwepa Ongata Rongai na huenda pia makubwa yake yakamfuata katika kanisa lake jipya .