Sonko kugharamia mazishi ya Kevin Oliech

Gavana wa Nairobi Mike Sonko  attoa sehemu ya gharama ya mazishi ya  Kevin Oliech ambaye aliaga dunia mwezi ulioppita .

Kevin  ni kakake mchezaji wa zamani wa Harambee Stars Denis Oliech na aliaga dunia kutokana na kansa  katika hospitali moja mjini Berlin ,Ujerumani agosti tarehe 16 mwaka huu .

Kupitia twitter , Sonko amesema atalipia baadhi ya gharama za mazishi ya Kevin . amesema alimjua marehemu kupitia kakake Denis  huku akimsifia kama mwanasoka stadi ka tu kaake Denis .

Kevin alizichezea timu za Nairobi City Stars kisha baadaye Mathare United .Mwili wake utawasili katika uwanja wa ndege wa JKIA  siku ya alhamisi .

Utahifadhiwa katika  Umash Funeral Home  kisha usafirishewe siku ya ijumaa  kwa mazishi Seme siku ya jumamosi .