Bangi ni dawa : Seneta Olekina ataka kuhalalishwa kwa bangi

ole kina
ole kina
Seneta wa Narok  Ledama Olekina  ametaka kuhalalishwa kwa bangi  ili itumie  katika matibabu .

Seneta huyo aliiweka video yake mtandaoni akiwa akatika shamba la bangi katika taifa la Lithuania .

Olekina  ambaye alikuwa nchini humo amesema iwapo Lithuania imehalalisha Bangi basi  Kenya pia inafaa kurekebisha sharia ili kuhalalisha mmea huo ili kuwapunguza makali wagonjwa hasa wa ugonjwa wa saratani .

“ Mbona Kenya bado tumesalia katika   msimamo wa zamani wa kuharamisha bangi …inanuka kama bangi..huenda nikalewa  huu ndani’ Ole Kina amesema katika video hiyo .

Alizidi kusema  “ iwapo mmea huu unaweza kupunguza  uchungu kwa wagonjwa wa kansa  basi tuuhalalishe ..ni kipi kibaya sana kuhusu mmea huu watu huishi mara moja tu’.

Mbunge wa  zamani wa Kibra marehemu Ken Okoth  alikuwa amepigania kuhalalishwa kwa bangi .Okoth aliwasilisha mswada wa kuthibiti  bangi bungeni mwaka wa 2018 ili kuhalalisha mea huo .

Seneta wa Nairobi Mike Sonko  aliasjhiria katika mazishi ya Okoth kwamba ingekuwa bora kuendleza kazi ya mbunge huyo kwa kuendelea kupigania kuhalalishwa kwa bangi  ili iweze kutumiwa kwa matibabu