Utalijua jiji! Tazama biashara na shughuli ambazo zilitumiwa kuwalaghai wakenya pesa

screen protector
screen protector
Kupenda pesa ama vitu vya haraka kuna gharama yake kama ambavyo wakenya walivyogundua katika miaka  na siku za hivi karibuni . Kuna makeke yaliyozuka na baadhi ya biashara au shughuli hizi na watu wengi wakapoteza hela zao kwa matumaini kwamba wangepata faida au kunufaika . Hebu  Tazama vitu ambavyo vilitumiwa kama chambo kuzipunja fedjha za watu wasiojua kwamba walikuwa wanalaghaiwa .

Pyramid schemes

Palitokea makundi mengi mengi ya kuchanghisha na kuweka pesa kama akiba na hata  mengine yakiahidi faida kwa kujisali nayo ili kuweka kiasi Fulani cha pesa baada ya muda Fulani . Pindi ilipojulikana kwamba watu wengi walikuwa kweli wamepokea faida , idadi hata Zaidi ya wakenya waliendelea kuziweka pesa zao katika mashirika hayo ambayo hakuna aliyejua mwanzoni kwamba yalikuwa ya walaghai .

Muda sio mrefu wamiliki wa mashirika hayo walifunga afisi zao na kukwepa na mamilioni ya pesa za wananchi . watu walipoteza akiba za miaka kadhaa kwani walitaraji kupata mafaao katika siu za baadaye .Kutoka mashirika kama vile DECI N na mengine ya akiba na mikopo ,wakenya wamekuwa waathiriwa wa kupunjwa fedha kupitia mipango kama hiyo ya kuzua  shauku

Quail/Tombo na mayai yake

Asiyekumbuka sifa za mayao ya ndege huyu na nyama yake ni nani? Miaka michache iliyopita kuana waliozuka na madai kwamba ndeghe huyu na mayai yake ni miradi ambayo ingeleta mapato mengi sana na maelfu ya watu walikimbia hata kuchukua mikopo kuana kuwafuga ndege hao . mwanzoni ikaonekana kana kwamba kweli kulikuwa na pesa lakini baadaye wakati mayai ya tombo yalipojaa sokoni na bei ikatumbukia ,kila mkulima wa ndege hawa alikuwa akilia machozi ya majuto lakini hakuna aliyekuwepo kumliwaza . Inadaiwa  waliokuja na   madai hayo walikuwa washatengeza pesa za kutosha na kujiendea zao

Liquid screen protector

Huko mitaani na vijijini umewaona watu na vijisanduku vyemnye kemikali inayodaiwa kuweka kwenye simu ili kulinda kioo chako . Mwanzoni ,watu walikuwa wakitoa hata shilingi 2000 kuwekewa kemikali hiyo  ya majimaji ili kuzikinga simu zao zisiweze kuvunjika vioo hata zikiangushwa . Kumbe wakati huo wote huu ni mchezo wa ulagjai na hadi leo kuna wakenya wasiojuwa kwamba  ‘kinga’ hiyo ya simu haisaidii nab ado wanalipa pesa ili kuwekewa katika simu zao za mkononi .

Maski

Mwanzoni mwa janga la corona ,maski ama barakoa ilikuwa mojawapo ya bidhaa zilizokuwa na gharama ya juu . kuna aina moja ya maski za  samawatu ambazo hutumiwa na madaktari ambazo ziliuzwa shilingi 300 mwanzoni mwa mwezi machi .Kufikia mwezi septemba maski hizo zilikuwa zikiuzwa shilingi tano! Maski zilipungua bei kw anjia ya kushangaza hadi imebainika kwamba kumbe kuna wafanyibiashara waliotumiua janga la corona kama chambo cha kujinufaisha kifedha .