"MImi na mke wangu ni watu wa hasira, tulikosana na mke wangu baada ya kusema kuwa nina mchunga sana hii ni baada ya kumpata anapigiwa simu na watualienda tu hapa Kawangware kwa mama yake, nimeenda mpaka kwao mwishowe mama yake aliniambia napaswa kuzungumza naye ninapozungumza naye ananiambia kuwa siwezi badilika
nilipokuwa namuoa alikuwa na watoto wawili, niliona ndoa yetu itakuwa kamili kwa maana hata mimi nina watoto nje." Alieleza Bwana Shem.
Moraa kwa upande wake alisema kuwa hataki kurudiana naye, huku akieleza alisema,
"Nilikuwa nikipigiwa simu ata kama sijui huyo mtu Shem ananigombanisha sidhani kama ni wivu kwa maana nikipigiwa na mama yangu alikuwa ananiambia heri singekuwa na mama
Nadhani mume wangu alikuja kugundua kuwa ananipenda baadaye lakini si mara ya kwanza ambapo alikuwa ananitaka kwa maana nilimpenda sana
Alikuwa pia anaambia watoto wangu kuwa yeye si baba yao na hata kuwaambia kuwa mimi nina wanaume wengi,ilifika mahali nikajiuliza kama mimi ndio mwanamume kwa uhusiano wetu."
Moraa alisimama na msimamo wake na kusema kuwa hayuko tayari kurudiana na Shem.