Katika hali ya kawaida na kutokana na mazoaea au mila na desturi , inafahamika kwamba mwanamme ndiye humtongoza mwanammke ,lakini usasa na kubadilika kwa mambo pamoja na teknolojia ni mambo ambayo yamesAwazisha uwanja na wanawake sasa wanapata ujasiri wa kuwakaribia wanaume na hata kuanza mchakato wa kuwajua na hata kuwatongoza .
Je ,ni vipi unavyoweza kuwa wa kwanza ‘kutupa mistari’ na kufaulu ?
Hatua kwa hatua
Siri unayofaa kufahamu kama mwanamke ni kwamba iwapo wewe utatangulia kuzungumza na mwanamme ambaye amekuvutia fahamu kwamba ni bora upige hatua moja hadi nyingine .Usije ukamshtukiza kwa kumwagia moyo wote wakati mmoja kwani hilo litampa mshtuko na atarudi nyuma .Mwanzo hakikisha kwamba mnafahamiana kama marafiki lakini unapozungumza naye hakikisha anafahamu kwamba kwa kweli unampa muda wako .Hilo litamuacha na fikra za picha na sura yako akilini na hata huenda akachukua mwongozo kutoka hapo na akumalizie kazi . ni heri kuanza kama rafiki yake na umkaribie hadi upate wepesi wa kumweleza kwamba anakuvutia ama unampenda kwa njia Zaidi ya urafiki
Ucheshi na kujiamini
Ingawaje kuna dhana kwamba wanaume hupenda kuwinda na hivyo basi wao ndio hupendelea kutongoza kwanza ,iwapo kama mwanamke unafahamu jinsi ya kumfanya apasue kicheko na ujiamini hata katika mazungumzo yako ,basi safari yako kuuteka moyo wake itakuwa rahisi sana .Kuna wanawake wenye uwezo wa kuzua bashaha katika nyuso za wanaume na wao hupata urahisi sana wa kuanza mchakato mzima wa kujinyakulia mwanamme .
Muulize maswali
Unapotaka kujua mengi kuhusu mwanamme ,yeye hupatwa na mwamko wa kutaka kujua mbona una hamu sana ya kumjua na hiyo ni njia tosha ya kumfahamiha kwamba upo na una nia Zaidi ya moja . Wanaume hupenda sana wakati mwanamke ana uchu wa kutaka kuwajua kwa undani na akiipokea vyema ishara hiyo ya maswali basi atafunguka na itakuwa rahisi wewe kuwasiliana naye .
Usijitupe
Wakati mwingine wanawake wanaovutiwa na wanaume huanza kupoteza utaratibu kwa sababu ya haya au kutojiamini na kujipata wakijitupa kwa mwanamme .Hilo bila shaka litampa hofu kwa sababu ataanza kushangaa umejitupa hivyo kwa wanaume wangapi hata kama sio kawaida yako kujipata katika hali kama hizo
Tabasamu
Tabasamu ni kitu kinachozungumza mengi na inafahamika kwamba tabasamu nzuri ya mwanamke hufungua roho hata ya mwaname ambaye kwa mbali anaweza kuonekana mkali au mgumu wa kuzungumza naye .Kama mwanamke jifunze ustadi wa kupiga tabasamu nadhifu sana ambayo inamuacha mwanamme hoi .Kuna wanawake waliopendwa kwa kutabasamu tu hata bila kutamka neno !