"Tulioana na mke wangu mwaka wa 2011, tumebarikiwa na watoto wanne,mke wangu alinipata nikitaka kumuingiza mpango wangu wa kandonimemuoma msamaha lakini amekataa, alienda kuodisha nyumbani mahali pengine,nilikuwa na mpango wa kando kwa maana mke wangu hajaweza kunitosheleza haki yangu
amekuwa akifanya kazi mpaka usiku anaingia kitandani saa nane usiku wakati ambao nataka kuamka na kuenda kutafuta kibarua."Libese aliongea
Lakini kwa kawaida kuna kitu ametuficha? haya basi wacha tuone vile mkewe alikuwa na ya kusema.
"Nimeishi na Libese tangu akiwa shule lakini kazi yake ni kuingia na kutoka si fahamu pesa zake vile anazitumia ni mimi nang'ang'ana na kufanya mahitaji yotembali na hayo amekuwa na mipango ya kando nyingi, analeta mwanamke mmoja baada ya mwingine wana lala naye kwa kitanda yetu
Mimi nikifanya makosa wazazi wake wananiita malaya akifanya makosa hawaoni makosa yake bali wananiekelea makosa yote,nimeishi naye huku akishinda kila wakati kusema atabadilisha tabia yake lakini hajabadilisha
mimi nahofia wanangu sitaki kuwaacha wangali wachanga kwa maana humu nje huwezi jua wala kufahamu mtu ambaye ana ugonjwa na hana."