Watu wengi hupatwa kighafla na janga hilo la kupoteza kazi na wataalam wanasema pindi unapopata kazi ,unafaa kuanza kujitarayrisha kwa siku ambayo kazi hiyo tafika mwisho .Kuanzia kuweka akiba hadi kujishughulisha na vyenzo vingine kwa kupata kipato -njia za kupunguza mshutuko na msonono unaotokana na kupoteza kazi ni nyingi na tumezijadili katika Podi hii
Ripoti mpya ya shirikisho la waajiri nchini FKE imeonyesha kwamba virusi vua corona vilisababisha kupotea kwa asilimia 80 ya kazi katika sekta ya kibinafsi tangu mwaka wa 2015
Matokeo ya utafiti huo yaliyotolewa wiki jana yanaonyesha kwamba jumla ya idadi ya wafanyikazi waliopungua katika kampuni zilizohojiwa ilipungua kutoka 406 hadi 372 ,upungufu wa asilimia 8.3 wa jumla ya idadi ya wafanyikazi .Akiitoa ripoti hiyo ,afisa mkuu mtendaji wa FKE Jacqueline Mugo amesema uchunguzi uligundua kwamba kulikuwa na matatizo ya uhaba wa fedha ,opareshenu na msururu wa usambazaji wa bidhaa na huduma uliathiriwa sana na janga la covid 19 .