Jumuiya ya EAC yampiga Jeki waziri Amina Mohamed katika ari yake ya kuwa mkurugenzi mkuu wa WTO

Amina
Amina
Baraza la mawaziri wa  Jumuiya ya afrika mashariki limeunga moono jitihada za waziri wa spotai Amina Mohammed kuwa mkurugenzi mkuu wa shirika la kimataifa la biashara WTO

Baraza hilo kupitia taarifa siku ya jumatatu kuimwidhinisha Amina ni  azimio linaoambatana na msimamo wa rais wa Rwnada Paul Kagame ambaye ndiye mwenyekiti wa baraza la marais wa Jumuiya ya Afrika mashariki anliyependekeza kwamba EAC imuunge mkono Amina kuipata kazi hiyo .

Taarifa hiyo imesema balozi Amina Mohammed ameidhinishwa kama  mgombeaji wa EAC kwa nafasi hiyo .

Wiki jana mshikilizi wa dunia wa rekodi yam bio za  Marathon Eliud Kipchoge  alimuidhinisha Amina kwa kazi hiyo .

Katika ujumbe wake wa kumuidhinisha , Kipchoge alisema  Amina ameonyesha weledi wa kufaulu hata  katika hali ngumu .