Michezo: Chelsea, Leicester zaandikisha ushindi, Ozil kuondoka Arsenal

Picha kwa hisani ya BBC
Picha kwa hisani ya BBC

Leicester ililaza Southampton 2-0 kupitia magoli ya James Madison na Harvey  Barnes katika kipindi cha kwanza  na kuhakikisha wamepanda hadi nafasi ya pili kwenye jedwali ya EPL, alama moja  nyuma ya Manchester United.

Kwingineko, Chelsea ililaza  Fulham 1-0 na kupanda hadi nafasi ya saba kwenye jedwali kupitia goli la pekee la  Mason Mount katika kipindi cha pili.

Katika matokeo mengine jana, Westham ililaza  Burnley 1-0 huku Leeds pia wakinyukwa  1-0 na Brighton, nao Wolves walipoteza  3-2 dhidi ya Westbrom, huku kocha  Sammy Allardyce akinyakua ushindi wake wa kwanza tangu kuchukua usukani mwezi uliopita.

Na Katika ligi kuu ya FKF Humu nchini, Tusker ilibwaga Kariobangi Sharks 4-2 na kupanda hadi nafasi ya pili alama moja nyuma ya viongozi KCB, huku Bandari nao wakipanda hadi nafasi ya nne baada ya kuwalaza Kalamega Homeboyz 4-3 ugani Mbaraki.

Kwingineko Nzoia Sugar ilinyuka  Sofapaka 2-1 na kandikisha ushindi wao wa kwanza msimu huku wanajeshi Ulinzi wakitoka sare ya 1-1 na City Stars.

Katika tetesi za soka duniani,Mesut Ozil yuko mbioni  kuondoka ugani Emirates baada ya kuchezea Arsenali kwa muda wa miaka saba.  

Mzaliwa huyo wa Ujerumani mwenye umri wa miaka 32 amekubali kujiunga na miamba wa Uturuki Fenerbahce kwa  muda wa miaka mitatu na nusu.  

Ozil hakua katika mipango ya kocha mkuu Mikel Arteta licha ya uzoefu wake na hajacheza mechi yoyote msimu huu.  

Kwa mujibu wa Fernabache,  the gunners watalipa marupurupu ya Ozil kwa miezi sita kama walivyokubaliana. Kwingineko, Nyota wa Bayern Munich Kingsley anadai  yuko sawa katika ligi ya Bundesliga,  na hatoondoka licha ya kuhusishwa na miamba wa Uingereza Manchester United na Man City.

Kiungo huyo wa Ufaransa  amekua katika hali dhabiti huku akifunga magoli  matano na kusaidia kufunga tisa, katika mechi  15.  

United  wamekua wakimmezea mate Kingsley  kwa muda mrefu  na huku Manchester City pia wakionyesha nia ya kumsajili.