•Nyakundi alimuita Atwoli mwizi na mlaghai
•Atwoli amekuwa katika mstari wa mbele kupigia debe BBI
Katibu mkuu wa COTU Francis Atwoli ametishia kumpeleka kotini mwanablogu Cyprian Nyakundi na kumuagiza atafute kazi aache kuwa mvivu.
Tishio hili limetokana na ujumbe ambao Nyakundi alichapisha siku ya Jumamosi akidai kuwa bwana Atwoli alikuwa na matumaini makubwa kuwa angepata kazi katika cheo cha juu zaidi nchini baada ya kupitisha mchakato wa BBI.
#BBICasualties : Conman of epic proportions and thief beyond measure Francis Atwoli had hoped to land an executive position in Government, through the botched BBI. He now retreats to his Namanga residence after emptying COTU coffers dry. pic.twitter.com/9ZzwkL45nB
— Cyprian, Is Nyakundi (@CisNyakundi) May 15, 2021
Kwenye ujumbe huo, Nyakundi alidai kuwa Atwoli alikuwa ameenda likizo kwenye makazi yake yaliyo Namanga baada ya kupora muungano wa COTU huku akimuita mlaghai na mwizi.
Akijibu ujumbe huo, Atwoli ambaye alionekana kashikwa na hasira alimwambia Nyakundi kuwa hatasita kumfanya atiwe mbaroni tena.
“Niko na kazi, sitafuti kazi nyingine. Umetiwa mbaroni hapo awali kwa kuchapisha madai yasiyo ya kweli kunihusu na nitafanya ukamatwe tena ili udhibitishe madai yako,” Atwoli alimwandikia Nyakundi.
I don't need a job in government. I already have a job. You have been arrested previously based on libel against me. And I will once again get you arrested to prove your claims.
— Francis Atwoli NOM (DZA), CBS, EBS, MBS. (@AtwoliDza) May 15, 2021
As an elder I advise you get a decent job(SDG 8). Get busy. Stop living a lazy & miserable life.
Bosi huyo wa COTU amekuwa kwenye mstari wa mbele katika kupigia debe mchakato wa BBI. Atwoli walionekana kukutana na kiongozi wa ODM Raila Odinga na naibu kiongozi wa chama cha Jubilee David Murathe baada ya mahakama kuu kutupilia mbali mchakato wa BBI.
Ingawa mada ya mkutano huo haijawekwa wazi, inashukiwa kuwa walikuwa wanajadili mipango ya namna wangesonga mbele na mchakato huo.
Mwanasheria mkuu wa serikali Bw Kihara Kariuki ametoa ilani ya kata rufaa maamuzi ya mahakama kuu kutupilia mbali mchakato wa BBI. Viongozi wanaoupigia debe mchakato huo wameendelea kusuta maamuzi ya koti.